Christmas Pilau

Click here to read in English
By Miriam
an image

Hili ni pilau tamu sana kwa sababu ya mchanganyiko wa korosho, zabibu kavu na zafarani. Wakati wa Noeli ni wakati wa vyakula vitamu vitamu, na mapishi haya ya pilau nimetengeneza kwa sababu hiyo tu. Ili pilau hii iwe inavyotakiwa, lazima utumie zafarani. Kama huna zafarani unaweza kutumia manjano.
Mlo huu ni wakuwatosha watu 6 au 8.

Viungo
Pilau Masala Other
  1. Bandika sufuria, tia mafuta kwenye moto wa kati. Ongeza mchele na vitunguu. Changanya mbaka mchele uwe mweupe na pia unachambuka chambuka.
  2. Ongeza kwenye sufuria vitunguu, tangawizi, na pilau masala. Endelea kuchanganya ili viungo visigande chini ya sufuria pia mbaka vitunguu swaumu viive. Ongeza zafarani.
  3. Kwenye chombo tofauti, changanya tui lamoto na mchuzi wa kuku wa moto.
  4. Ongeza mchanganyiko huo wa nazi kwenye sufuria ya mchele ulio jikoni.
  5. Funika sufuria halafu punguza moto uwe kati ya moto wa katikati na wachini. Maji kama yakikauka ongeza korosho, changanya vizuri halafu ongeza nusu kikombe cha mchuzi wa kuku. Onja uone kama chumvi inatosha.
  6. Kama pilau ikikaribia kuiva, ongeza zabibu kavu, majani ya mgiligilani. Changanya vizuri, funika endelea kupika au weka kwenye oveni kama 300F mbaka ukauke vizuri.
  7. Weka mezani wakati bado pilau lina moto.